SHAMBA LA BIBI

SHAMBA LA BIBI

Friday, 14 August 2015

POLISI MBEYA WAPIGA MARUFUKU MAANDAMANO WAKATI WA KUMPOKEA MGOMBEA UKAWA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limepiga marufuku maandamano wakati wa kumpokea Mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mh. Edward Lowassa, hii leo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (ACP) Ahmed Msangi ametoa agizo hilo kwa wananchi kutofanya maandamano yoyote yawe ya miguu au pikipiki na kusema kuwa kibali chao ni mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe kinyume na hapo polisi itachukua hatua kali za kisheria.


No comments:

Post a Comment