Wizara ya afya nchini kenya imetoa orodha ya peremende, keki na biskuti bidhaa ambazo inadai zimewekwa bangi.
Katika kile ambacho kinatarajiwa kuwashangaza wazazi, barua ambayo ilitiwa sahihi kwa niaba mahabara ya serikali, ilisema kuwa baadhi ya sampuli 176 zilizochukuliwa kwa peremende maarufu , keki na mandazi zilipatikana zikiwa na bangi baada ya kufanyiwa uchunguzi.
Kupitia kwa barua kwenda kwa wakuu wa afya wa kaunti zote 47 nchini Kenya, wizara ya afya imewaamrisha maafisa kukagua maduka yote, maduka ya jumla na sehemu zingine bidha hizo zinaweza kupatikana.
Source: BBC Swahili.
No comments:
Post a Comment