SHAMBA LA BIBI

SHAMBA LA BIBI

Friday, 14 August 2015

Huyu ndiye Mrithi wa Kiongozi aliyetimuliwa kazi na Ban Ki–moon

Parfait Onanga-Anyanga
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki -moon amemteuwa Parfait Onanga-Anyanga, raia wa Gabon, kuwa mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, baada ya kumtimua kazi Babacar Gaye (kutoka Senegal) kufuatia kashafa za ngono zinazokisiwa kutekelezwa na walinda amani umoja wa mataifa nchini Afrika ya Kati.
Ban Ki-moon pia ameongeza kutilia mkazo sera zake za kutovumilia makosa yanayotuhumiwa vikosi vya majeshi ya Umoja wa Mataifa, hususan kashfa za ngono, wakati ambapo shutuma za uhalifu wa kijinsia dhidi ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa zimekua nyingi miaka ya hivi karibuni.

Babacar Gaye (aliyetimuliwa)

No comments:

Post a Comment